BARAZA LA TAIFA LA ELIMU YA UFUNDI
(NACTE)
TAARIFA KWA UMMA
KUFUNGULIWA KWA MFUMO WA PAMOJA WA UDAHILI KWA KIPINDI CHA MACHI/APRILI, 2017 KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE), linapenda kuutangazia Umma na wadau wote wa Elimu nchini, kuwa mfumo wa Udahili wa pamoja yaani “Online Central Admission System (CAS)”, umefunguliwa rasmi tarehe 23 Januari, 2017, saa 6 mchana, kwa kupokea maombi ya mwombaji katika kozi mbalimbali, ikiwemo ngazi ya, Astashahada na Stashahada kwa Kipindi cha Machi/April, 2017 kwa mwaka wa masomo 2016/2017.
Namna ya Kufanya Maombi
Maombi yote yafanyike kupitia Mfumo wa Udahili wa Pamoja (CAS) au kupitia chuoni ambapo mwombaji anapendelea kwenda kusoma, ambapo chuo kitamdahili mwanafunzi husika kwenye mfumo wa udahili kupitia “Institutional Panel”.
Tanbihi: Waombaji wa kozi za Afya waliohitimu Astashahada (NTA Level 5), pia wataomba kwa utaratibu ulioelezwa hapo juu.
Mwombaji wa Astashahada na Stashahada anaweza kuomba kwa ajili ya eneo moja au zaidi katika maeneo ya taaluma yafuatayo:
- Biashara, Utalii na Mipango, mfano; Uhasibu, Meneja Rasilimali Watu, Wanyama Pori, Mipango.
- Sayansi na Teknolojia Shirikishi, mfano; Kilimo, Uhandisi, Mifumo ya Mawasiliano, Usanifu Majengo, Mifugo.
- Afya na Sayansi Shirikishi, mfano; Uganga, Maabara, Ufamasia, Uuguzi.
Sifa za muombaji
- Awe amehitimu kidato cha nne mwaka 2015 au kabla ya hapo.
- Awe na Astashahada ya mwaka 2016 au kabla ya hapo kwa wanaojiendeleza.
- Sifa kwa kozi mahsusi ziko kwenye mwongozo wa kozi (Guidebook) ulioko kwenye mfumo (CAS).
Ada ya maombi ni kama ifuatavyo:
- Kwa eneo la Afya na Sayansi Shirikishi ada ya maombi ni Tshs 30,000/=.
- Kwa eneo moja kati ya maeneo mengine yaliyobaki, ada ni Tshs 20,000/=.
- Kwa zaidi ya eneo moja la taaluma, mfano; Afya pamoja na Biashara, ada ni Tshs 30,000/=, ambapo muombaji anaruhusiwa kuchagua maeneo yote.
Mwisho wa kutuma maombi haya ni tarehe 06/03/2017.
Muhimu: Hakutakuwa na muda wa nyongeza wa kufanya maombi. Hivyo waombaji wanashauriwa kuwa makini wakati wa kufanya maombi yao.
BOFYA HAPA KUPATA ORODHA YA VYUO
Imetolewa na:
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
23 Januari, 2017
Je, vyuo vya maendeleo ya jamii vimesha anza udahili wa mwaka wa masomo 2018/2019?
LikeLike
Udahili wa kada ya elimu lini??? Mwez Wa tano ndio huu
LikeLike
Bado mamlaka zinazohusika zipo kimya, endelea kuwa nasi kwa taarifa yoyote itakayotolewa
LikeLike
Mie nataka taarifa za udahili kada ya elimu,,, halafu hizo taarifa zimesha expire ndio zinanifikia kma ningekuwa mlengwa mngenisaidiaje
LikeLike
Habari Mulhat!
Unaweza kurudia swali lako vizuri, una maanisha udahili wa walimu umekwisha fungwa?
LikeLike
Mfumo Wa Udahili Utafunguliwa Lini Tena Kwa Mwaka Wamasomo 2017/2018
LikeLike
Bado haujafunguliwa, endelea kuwa nasi kwa taarifa mara tu utakapokuwa umefunguliwa
LikeLike
Naomba nitumie listi ya vyuo vya serikali vinavotoa diploma in primary,,,, Tafadhali
LikeLike
Udahili katika kada ya elimu lini?? ?tujuzeni mapema
LikeLike
Kwa kawaida huwa ni may, ila tuendelee kusubili mamlaka husika NACTE watakapofungua dirisha la udahili tutawajulisha.
LikeLike
Mimi naomba kujua kama kutakuwa na udahili mwingine katika vyuo vya kilimo kwa ngazi ya Diploma mwaka 2017/2018?
LikeLike
Endelea kutufuatilia, ukiwepo tutawajulisha hapahapa bila kukawia
LikeLike
je kwa wale walioitim kidato cha nne 2016 udahili wao ni lini
LikeLike
Kuanzia mwezi July hadi Oktoba kutegemeana na tangazo la NACTE litakavyotoka
LikeLike
kwa wahitimu wa kidato cha nne 2016 wanatakiwa kuanza kufanya maombi ya kudahiliwa mda gani? .na nilini wanatakiwa kuanza kufanya maombi?
LikeLike
Waliomaliza 2016 watadahiliwa mwezi wa kumi, tarehe ya kutuma maombi itatangazwa na mamlaka husika (NACTE). Endelea kututembelea utapata taarifa watakapofungua dirisha la udahili
LikeLike
mbona nasikia kuna baadhi ya vyuo vilivyo sajiliwa na (NACTE) pia vina Dahili wanafunzi mwezi wa saba (7)
mfano: chuo cha JORDAN UNIVERSITY COLLEGE (morogoro)
Au kila chuo kinataratibu zake za kudahili wanafunzi???
LikeLike
napendekeza mngetoa kitabu cha muongozo waombaji wakione kabla hawaja anza kuomba pia naomba kutumiwa vigezo vya kujiunga na nursing pamoja na pharmacy kwa wanaohitaji kusoma ngaz ya cheti
LikeLike
Kozi yoyote ya cheti inahitaji uwe na ufaulu usiopungua D nne za kidato cha nne, kwa msaada zaidi bofya “Kutafuta chuo/shule” kwenye menyu yetu hapo juu
LikeLike